0
Image result for contract
Mkuu wa Wilaya ya Kinondini, Ally Hapi amesema atawafutia leseni wamiliki wa hoteli na kampuni binafsi ambao hawajatoa mikataba ya ajira kwa wafanyakazi wao.

Aliwabana wamiliki hao jana alipokuwa katika ziara wilayani humo na kutembelea baadhi ya hoteli na kampuni binafsi kwa lengo la kuzungumza na wafanyakazi.

Awali, wafanyakazi walilalamikia mazingira magumu ya kazi ikiwamo mishahara duni na kufanya kazi bila mikataba.

Mmoja kati ya wafanyakazi 23 wa Hoteli ya Tangren iliyopo Mikocheni, Lilian Semtanda alisema licha ya kufanya kazi kwa miaka mitano, hajapatiwa mkataba huku akinyimwa stahiki ikiwamo likizo na matibabu.

Hata hivyo, mmiliki wa hoteli hiyo, Liu Dengwei alikiri kutotoa mikataba tangu waanze mwaka 2008 lakini wameanza utekelezaji wiki hii.

Post a Comment

 
Top