1. Simon Msuva. Mcheza soka katika timu ya taifa Taifa Stars na pia winga
wa klabu ya Yanga Simon Msuva anaongoza orodha hii, Msuva hadi sasa ana
followers 207,000 na ndio mchezaji anayeongoza akiwa amewaacha wenzake
kwa mbali sana.
2. Juma Kaseja. Golikipa wa Kagera Sugar ambaye pia amepitia vilabu vya
Yanga na Simba Juma Kaseja yuko nafasi ya pili akiwa na idadi ya
followers 115,000 katika ukurasa wake wa Instagram.
3. Haruna Nyionzima. Wakati Msuva anaongoza kwa idadi ya followers
instagram anayemfuatia kwa idadi kubwa ya followers kutoka Yanga ni
Haruna Nyionzima, Mnyarwanda huyo hadi sasa ana idadi ya followers
114,000 katika ukurasa wake wa Instagram.
4. Deus Kaseke. Yanga tena wanakuja katika nafasi ya nne hii inamaanisha
nne bora ni mchezaji mmoja tu asiyetokea Yanga, Kaseke yupo katika
nafasi hii akiwa na followers 109,000 katika ukurasa wake wa Instagram.
5. Paul Nonga. Mshambuliaji wa Mwadui Fc anatokea katika nafasi ya tano,
huyu ni Nonga ambapo Nonga ana followers 101,000 katika ukurasa wake wa
Instagram
6. Juma Abdul. Nafasi ya 6 pia ni Yanga, Juma Abdul yuko katika nafasi
hii kwa kuwa na followers 96,800 katika ukurasa wake huo wa Instagram.
7. Mohamed Hussein. Nafasi ya saba ndio kumetokea mchezaji wa kwanza
ambaye ni Simba na ni beki wa Simba Mohameid Hussein Tshabalala ambaye
ana idadi ya followers 96,200 katika ukurasa wake wa Instagram.
8. Said Ndemla.Kiungo wa Simba Saidi Hamisi Ndemla yuko katika nafasi ya 8
akiwa ana followers 81,900 ikiwa ni pungufu ya followers 14,300 kutoka
alipo Tshbalala.
9. Mrisho Ngassa. Nafasi ya tisa inashikiliwa na winga wa zamani wa
klabu ya Yanga ambaye kwa sasa anakipiga Mbeya City Mrisho Ngassa.
Ngassa anao followers 88,700 katika mtandao wake wa Instagram.
10. Himid Mao. Nafasi ya 10 ni kiungo mkabaji wa Azam Fc Himid Mao
“Ninja”, Himid ameingia katika kumi bora ya wasakata kabumbu wa Tanzania
wenye followers wengi akiwa na followers 74,400.
Post a Comment