Pichani Balozi Asha Rose Migiro akipokea Fulana hiyo.
Balozi wa Tanzania nchini Uingereza, Dkt. Asha - Rose Migiro leo
aliandaa hafla fupi katika makazi ya Balozi kumpongeza kijana mtanzania
Alphonse Simbu alieshika nafasi ya tano katika mbio za "London Marathon"
zilizofanyika tarehe 23 Aprili 2017 jijini London.
Katika salamu zake, Balozi Migiro alimpongeza Bw. Simbu kwa
heshima aliyoipa Tanzania jijini London na Duniani kupitia mbio za
London. alimsihi atumie matokeo hayo kama hamasa ya kufanya bidii zaidi
kwa ajili ya mashindano ya mbio ndefu anayotarajiwa kushiriki baadae
mwakani.
Simbu alimshukuru Balozi Migiro Kwa ushirikiano mkubwa wa kibalozi
alioupata akiwa jijini London.Alimkabidhi Balozi Fulana ya kumbukumbu
ya ushiriki wake kwenye mbio hizo.
Post a Comment