“Tumejitahidi kwenye Game lakini wenzetu wamepata nafasi, wameitumia
na hii ndio Football, ila tunajipanga upya na tunakubali matokeo”,”This
is Football kwa sababu wametengeneza nafasi na ikapatikana ushindi, so
huwezi kuulaumu sana”. Nahodha huyo amewataka mashabiki na wanachama wa klabu ya Yanga
kuelekeza nguvu yao katika ligi, kwa sababu bado wana nafasi ya
kuiwakilisha nchi katika anga za kimataifa kupitia Ubingwa wa ligi kuu
ya Vodacom.
Nae nahodha wa klabu ya Mbao Fc Ndikumana , amekiri kuwa Yanga ni
timu nzuri, ila ushindi wao unatokana na Umoja waliokuwa nao ndani ya
klabu na hivyo ndivyo watakavyocheza hata wakikutana na klabu ya Simba
Sc.
Katika mchezo huo, klabu ya soka ya Yanga imevuliwa taji la pili
msimu huu, baada ya kutupwa nje ya michuano ya Kombe la Shirikisho la
Soka Tanzania (TFF), inayojulikana kama Azam Sports Federation Cup
(ASFC), kufuatia kipigo cha 1-0 wao wakiwa ndio Mabingwa watetezi Mchezo
uliopigwa katika Dimba la CCM Jijini , Mwanza.
Post a Comment